forjoys
Thursday, February 21, 2013
Wednesday, September 14, 2011
HIVI NDIVYO NDEGE ILIVYO UMIA BAADA YA KUANGUKA ENEO LA NANE NANE UYOLE MBEYA
HABARI KAMILI
Ajali ya ndege namba 9J-BIO SESINA 206, imetokea leo asubuhi majira ya saa tatu eneo la Nanenane Uyole jijini Mbeya na abiria wanne wanusurika kifo na hakuna aliyefariki.
NDEGE INAVYO ONEKANA BAADA YA KUPATA AJALI...
BAADHI YA WATU WALIO FIKA ENEO HILO LA TUKIO KUTOA MSAADA BAADA YA AJALI HIYO.
PICHA ZOTE NA MBEYA YETU BLOG
Sunday, September 11, 2011
Saidiazanzibar - We need your help
PRESS RELEASE
On Friday 10th September 2011, the ferry M.V. Spice Islander, travelling between Dar es Salaam, Zanzibar, Pemba and Tanga, capsized in deep waters in the Pemba Channel, north of Zanzibar island.
The true numbers of those injured or dead in the tragedy has yet to be established, but it is now acknowledged that there were many more passengers than the 610 listed on the ship manifest. As of Saturday night, 200 are dead, 500 have been rescued and many are still missing. The full extent of the tragedy will not be known for several more days.
Saidia Zanzibar (www.saidiazanzibar.org) is an emergency fundraising website, to provide caring members of the public, in Zanzibar and the world at large, with a framework to commit some of their time and money for the assistance of those tragically affected by the disaster.
We will be posting updates in the coming days, including a Zanzibar bank account to which money can be sent, and details of those organizations to whom the money will be subsequently disbursed on your behalf.
The fundraising effort will be overseen by the Zanzibar Association of Tourism Investors (www.zati.org), a registered NGO, who will co-ordinate donations and offers of assistance from their office located in the Cine Afrique in Malindi, Stone Town, Zanzibar.
Further updates will be posted throughout the period starting 12th September 2011. Email enquiries can be sent to saidia@saidiazanzibar.org.
Zitto Kabwe Anaelezea Hisia Zake Juu Ya Msiba Mkubwa Wa Kitaifa
by Zitto Z Kabwe on Sunday, 11 September 2011 at 16:19
(Nimeandika makala hii nikiwa katika Benchi la Hospitali ya Mnazi
Mmoja hapa Zanzibar. Mniwie radhi kama kuna spelling mistakes kwani
nilitaka hisia zangu ziwe as raw as possible - Zitto Zitto and not
Zitto a Politician).
Jana asubuhi tarehe 10 Septemba 2011 Taifa liligubikwa na habari za
kushtusha za maafa. Mwanzoni taarifa zilisambaa kwamba zaidi ya watu
2000 walikuwa kwenye Boti MV Spice Islander lililopinduka na kuzama
mbele kidogo ya Nungwi likielekea kisiwani Pemba. Habari hazikuwa za
uhakika sana kwani vyombo vyetu vya habari na hasa Televeshini ya
Taifa havikuwa vikitoa habari juu ya ajali hii.
Habari zilisambaa kupitia mitandao ya intaneti na kufuatia uchu wa
habari nilianzisha #ZanzibarBoatAccident katika mtandao wa twitter ili
tuweze kufuatilia kwa karibu habari zote za ajali hii.
Habari zilisambaa kuwa Televisheni ya Taifa ilikuwa inaonyesha muziki
wa Taarab na Baadaye vipindi vingine vya kawaida bila kutoa habari kwa
Umma kuhusu msiba huu.
Watanzania waliokoa wakiwasiliana kupitia twitter na facebook walikuwa
na hasira sana na kituo cha TBC1 kutoonyesha au kupasha habari juu ya
ajali hii. Mpaka saa moja jioni kituo hiki cha Televisheni ya Taifa
kilikuwa kinaonyesha watu wakicheza muziki wa Kongo, wanawake
wakikatika viuno na hata ngoma za asili.
'Hallo, washa TBC1 uone Televisheni yenu inachoonyesha' yalikuwa ni
maneno ya Mwakilishi Ismael Jussa Ladhu aliponipigia kuonyesha
kusikitishwa kwake na kituo hiki. Mpaka jioni tulikuwa tumepata
taarifa kuwa Watanzania wenzetu 198 walikuwa wamepoteza maisha. 570
hivi walikuwa wameokolewa.
Binafsi nilipotembelea Hospitali ya Mnazi Mmoja niliweza kumwona Binti
aliyeitwa Leyla, akisoma darasa la Nne huko kisiwani Pemba. Leyla
alipona, aliokolewa. Nilimwambia leyla atapona na kurudi Shuleni.
Mpaka ninapoandika tumeambiwa kuwa Watanzania 240 wamegundulika
kupoteza maisha na zaidi ya 600 wameokolewa.
Napenda kuwapongeza sana waokoaji wetu, wavuvi wa kijiji cha Nungwi na
vijiji jirani, wamiliki wa mahoteli waliojitolea vifaa vyao kwenda
kuokoa watu na wanajeshi wetu wa majeshi ya ulinzi na usalama kwa kazi
hii kubwa ya kuokoa. Kwa kweli tumeokoa watu wengi kuliko
ilivyotarajiwa. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imejitahidi sana,
ilitulia na kuonyesha uongozi thabiti katika juhudi za uokoaji.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akafuta ziara yake huko
Canada, ziara iliyokuwa imeandaliwa muda mrefu na kwa gharama. Lakini
Rais aliona ni vema kupata hasara kuliko kuwa nje ya Nchi kipindi
hiki. Hakutaka hata kumtuma Makamu wa Rais au Waziri Mkuu. Alifuta.
Akatangaza siku 3 za kuomboleza.
Hata hivyo waandaaji wa Miss Tanzania waliona hasara kubwa kuahirisha
shindano la Urembo usiku huo. Wangepata hasara! Hata wafadhili wao
Kampuni ya simu za mkononi ya vodacom ambao miongoni mwa waliofariki
wamo wateja wa vodacom, waliendelea na shindano hili.
Jumatatu, tarehe 12 Septemba 2011 ni siku ya khitma ya kuwaombea marehemu wetu.
Nimeamua kutotumia simu yangu ya Voda kwa siku nzima, sina njia ya
kuiadhibu Kampuni hii isipokuwa kugoma kutumia simu yao japo kwa siku
moja kuonyesha kutoridhishwa kwangu na uamuzi wao wa kutojali msiba
huu kwa Taifa.
Misiba huweka jamii pamoja. Msiba huu uliotokea Zanzibar ni jaribio
kubwa kwa Umoja wa Taifa letu. Shirika la Utangazaji la Taifa
limeshindwa jaribio hili la kudhihirisha Umoja wetu katika kipindi
hiki. Nataraji wakubwa wa Shirika hili linaloendeshwa kwa kodi
watawajibika au kuwajibishwa!
Jumla ya Majeruhi na marehemu sasa inafikia zaidi ya Abiria 800!
Asubuhi ya jana 10 Septemba 2011 tuliambiwa na Serikali kwamba uwezo
wa Boti la MV Spice Islander ilikuwa ni abiria 500 na wafanyakazi 12.
Pia tumejulishwa kuwa boti hili lilikuwa la Mizigo na sio la Abiria.
Natumai mara baada ya kumaliza maombolezo haya ya siku tatu Wakuu wa
Mamlaka zinazohusika na usafiri wa Majini wa Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar watawajibika au kuwajibishwa. Mkuu wa Bandari ya Zanzibar
Mustafa Aboud Jumbe na Waziri wa Miundombinu Hamad Masoud wanapaswa
kufukuzwa kazi mara moja kama hawatawajibika wenyewe kwa kujiuzulu.
Kufukuzwa kwao kazi hakutarudisha ndugu zetu duniani bali itakuwa ni
somo kuwa hatutarudia tena kufanya makosa yaliyoleteleza ajali kama
hii.
Mwenyezi Mungu atupe subira wakati huu wa msiba mkubwa katika Taifa
letu. Alaze roho za marehemu wetu mahala pema peponi na awape unafuu
wa haraka majeruhi wetu.
Zitto Kabwe, Mb
Saturday, September 10, 2011
Ahadi Ya Ngeleja Yaongeza Machungu Mgawo Wa Umeme
Friday, September 9, 2011
TEMEKE KINONDONI NANI ZAIDI KATIKA MASUMBWI
MABONDIA Mbwana Matumla wa Temeke na Francis Miyeyusho wa Kinondoni Dar es Salaam wanatarajia kupanda ulingoni katika pambano la kudhihirishiana ubabe kati ya mabondia wa Temeke na Kinondoni litakalofanyika Oktoba 30 mwaka huu.
Pambano hilo pia litafuatiwa na lingine kati ya Ramadhani Shauri wa Kinondoni dhidi ya Issa Sewe wa Temeke ambapo yote yatafanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Kocha Msaidizi wa Kambi ya Kinyogoli Foundation ya Dar es Salaam, Rajabu Mhamila 'Super D' alisema mapambano hayo yameandaliwa na Promota Mohamedi Bawaziri kuhamashisha mchezo huo.
"Mabondia wote wameanza mazoezi na kwa upande wa Temeke wapo kambini chini ya Kinyogori Foundation chini ya kocha Habibu Kinyogori akishirikiana na mimi na tunawaandaa kucheza ngumi za kisasa sio kurusha ngumi bila mpangilio.," alitamba Super D
Alisema pambano kati ya Matumla na Miyeyusho litakuwa la uzani wa Bantam Weight kilogramu 54 ambapo Shauri na Sewe watacheza kilogramu 58, uzito mwepesi (Light Weight).
Alisema licha ya kuhamasisha, kumekuwepo na tambo za mda mrefu kati ya mabondia wa Kinondoni, na wenzao wa Temeke ambapo mashabiki watajionea mapambano hayo.
Kocha huyo alisema mapambano hayo yatasindikizwa na mengine kutoka kwa mabondia wa Temeke na Kinondoni ambapo pia kutakuwepo na burudani mbalimbali zitakazotangazwa baadae.
--
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
Mob;+255787 406930
Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania
Wednesday, September 7, 2011
Mchezaji Nazir Khalfan Atinga Ikulu Kumshukuru Rais Jakaya Kikwete na Kumkabidhi Jezi



Subscribe to:
Posts (Atom)