Wednesday, September 14, 2011

HIVI NDIVYO NDEGE ILIVYO UMIA BAADA YA KUANGUKA ENEO LA NANE NANE UYOLE MBEYA



HABARI KAMILI 
Ajali ya ndege namba  9J-BIO SESINA 206, imetokea leo asubuhi majira ya saa tatu eneo la Nanenane Uyole jijini Mbeya  na abiria wanne wanusurika kifo na hakuna aliyefariki.

Abiria walionusurika kifo ni pamoja JVER WAAK Umri wa Miaka 49 ambayealikuwa Rubani, Raia wa Afrika Kusini, Bwana CHRISTIAN BASIL MMASI umri miaka 30, Ambaye ni Afisa Utawala wa mashamba ya Kapunga wilaya ya Mbarali, Balozi MOHAMMED RAMIA kabula leke ni Mmakua mwenye umri wa miaka 64, mkazi wa Masaki jijini Dar es Salaam ambaye ni mfanyakazi EXPORT TRADING na Bwana SUNNY TAYIR mwenye umri wa miaka 50 ambaye ni Mhindi na ni mfanyakazi wa EXPORT TRADING.

Na chanzo cha ajali hiyo akijafahamiaka mpaka sasa.

Imetolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya Bwana ANACLET MALIMBISA
 NDEGE INAVYO ONEKANA BAADA YA KUPATA AJALI...

  BAADHI YA WATU WALIO  FIKA ENEO HILO LA TUKIO KUTOA MSAADA BAADA YA AJALI HIYO.

PICHA ZOTE NA MBEYA YETU BLOG

Sunday, September 11, 2011

Saidiazanzibar - We need your help


PRESS RELEASE

On Friday 10th September 2011, the ferry M.V. Spice Islander, travelling between Dar es Salaam, Zanzibar, Pemba and Tanga, capsized in deep waters in the Pemba Channel, north of Zanzibar island. 

The true numbers of those injured or dead in the tragedy has yet to be established, but it is now acknowledged that there were many more passengers than the 610 listed on the ship manifest. As of Saturday night, 200 are dead, 500 have been rescued and many are still missing. The full extent of the tragedy will not be known for several more days. 

Saidia Zanzibar (www.saidiazanzibar.org) is an emergency fundraising website, to provide caring members of the public, in Zanzibar and the world at large, with a framework to commit some of their time and money for the assistance of those tragically affected by the disaster.

We will be posting updates in the coming days, including a Zanzibar bank account to which money can be sent, and details of those organizations to whom the money will be subsequently disbursed on your behalf. 

The fundraising effort will be overseen by the Zanzibar Association of Tourism Investors (www.zati.org), a registered NGO, who will co-ordinate donations and offers of assistance from their office located in the Cine Afrique in Malindi, Stone Town, Zanzibar.

Further updates will be posted throughout the period starting 12th September 2011. Email enquiries can be sent to saidia@saidiazanzibar.org.

Zitto Kabwe Anaelezea Hisia Zake Juu Ya Msiba Mkubwa Wa Kitaifa

|
Taifa Msibani, Umoja wetu na Utu wetu Shakani
by Zitto Z Kabwe on Sunday, 11 September 2011 at 16:19

(Nimeandika makala hii nikiwa katika Benchi la Hospitali ya Mnazi

Mmoja hapa Zanzibar. Mniwie radhi kama kuna spelling mistakes kwani
nilitaka hisia zangu ziwe as raw as possible - Zitto Zitto and not
Zitto a Politician).

Jana asubuhi tarehe 10 Septemba 2011 Taifa liligubikwa na habari za

kushtusha za maafa. Mwanzoni taarifa zilisambaa kwamba zaidi ya watu
2000 walikuwa kwenye Boti MV Spice Islander lililopinduka na kuzama
mbele kidogo ya Nungwi likielekea kisiwani Pemba. Habari hazikuwa za
uhakika sana kwani vyombo vyetu vya habari na hasa Televeshini ya
Taifa havikuwa vikitoa habari juu ya ajali hii.

Habari zilisambaa kupitia mitandao ya intaneti na kufuatia uchu wa

habari nilianzisha #ZanzibarBoatAccident katika mtandao wa twitter ili
tuweze kufuatilia kwa karibu habari zote za ajali hii.

Habari zilisambaa kuwa Televisheni ya Taifa ilikuwa inaonyesha muziki

wa Taarab na Baadaye vipindi vingine vya kawaida bila kutoa habari kwa
Umma kuhusu msiba huu.

Watanzania waliokoa wakiwasiliana kupitia twitter na facebook walikuwa

na hasira sana na kituo cha TBC1 kutoonyesha au kupasha habari juu ya
ajali hii. Mpaka saa moja jioni kituo hiki cha Televisheni ya Taifa
kilikuwa kinaonyesha watu wakicheza muziki wa Kongo, wanawake
wakikatika viuno na hata ngoma za asili.

'Hallo, washa TBC1 uone Televisheni yenu inachoonyesha' yalikuwa ni

maneno ya Mwakilishi Ismael Jussa Ladhu aliponipigia kuonyesha
kusikitishwa kwake na kituo hiki. Mpaka jioni tulikuwa tumepata
taarifa kuwa Watanzania wenzetu 198 walikuwa wamepoteza maisha. 570
hivi walikuwa wameokolewa.

Binafsi nilipotembelea Hospitali ya Mnazi Mmoja niliweza kumwona Binti

aliyeitwa Leyla, akisoma darasa la Nne huko kisiwani Pemba. Leyla
alipona, aliokolewa. Nilimwambia leyla atapona na kurudi Shuleni.
Mpaka ninapoandika tumeambiwa kuwa Watanzania 240 wamegundulika
kupoteza maisha na zaidi ya 600 wameokolewa.

Napenda kuwapongeza sana waokoaji wetu, wavuvi wa kijiji cha Nungwi na

vijiji jirani, wamiliki wa mahoteli waliojitolea vifaa vyao kwenda
kuokoa watu na wanajeshi wetu wa majeshi ya ulinzi na usalama kwa kazi
hii kubwa ya kuokoa. Kwa kweli tumeokoa watu wengi kuliko
ilivyotarajiwa. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imejitahidi sana,
ilitulia na kuonyesha uongozi thabiti katika juhudi za uokoaji.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akafuta ziara yake huko

Canada, ziara iliyokuwa imeandaliwa muda mrefu na kwa gharama. Lakini
Rais aliona ni vema kupata hasara kuliko kuwa nje ya Nchi kipindi
hiki. Hakutaka hata kumtuma Makamu wa Rais au Waziri Mkuu. Alifuta.
Akatangaza siku 3 za kuomboleza.

Hata hivyo waandaaji wa Miss Tanzania waliona hasara kubwa kuahirisha

shindano la Urembo usiku huo. Wangepata hasara! Hata wafadhili wao
Kampuni ya simu za mkononi ya vodacom ambao miongoni mwa waliofariki
wamo wateja wa vodacom, waliendelea na shindano hili.

Jumatatu, tarehe 12 Septemba 2011 ni siku ya khitma ya kuwaombea marehemu wetu.


Nimeamua kutotumia simu yangu ya Voda kwa siku nzima, sina njia ya

kuiadhibu Kampuni hii isipokuwa kugoma kutumia simu yao japo kwa siku
moja kuonyesha kutoridhishwa kwangu na uamuzi wao wa kutojali msiba
huu kwa Taifa.

Misiba huweka jamii pamoja. Msiba huu uliotokea Zanzibar ni jaribio

kubwa kwa Umoja wa Taifa letu. Shirika la Utangazaji la Taifa
limeshindwa jaribio hili la kudhihirisha Umoja wetu katika kipindi
hiki. Nataraji wakubwa wa Shirika hili linaloendeshwa kwa kodi
watawajibika au kuwajibishwa!

Jumla ya Majeruhi na marehemu sasa inafikia zaidi ya Abiria 800!

Asubuhi ya jana 10 Septemba 2011 tuliambiwa na Serikali kwamba uwezo
wa Boti la MV Spice Islander ilikuwa ni abiria 500 na wafanyakazi 12.
Pia tumejulishwa kuwa boti hili lilikuwa la Mizigo na sio la Abiria.

Natumai mara baada ya kumaliza maombolezo haya ya siku tatu Wakuu wa

Mamlaka zinazohusika na usafiri wa Majini wa Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar watawajibika au kuwajibishwa. Mkuu wa Bandari ya Zanzibar
Mustafa Aboud Jumbe na Waziri wa Miundombinu Hamad Masoud wanapaswa
kufukuzwa kazi mara moja kama hawatawajibika wenyewe kwa kujiuzulu.

Kufukuzwa kwao kazi hakutarudisha ndugu zetu duniani bali itakuwa ni

somo kuwa hatutarudia tena kufanya makosa yaliyoleteleza ajali kama
hii.

Mwenyezi Mungu atupe subira wakati huu wa msiba mkubwa katika Taifa

letu. Alaze roho za marehemu wetu mahala pema peponi na awape unafuu
wa haraka majeruhi wetu.

Zitto Kabwe, Mb

Saturday, September 10, 2011

Ahadi Ya Ngeleja Yaongeza Machungu Mgawo Wa Umeme

MATUMAINI yaliyotolewa na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kwamba makali ya mgawo wa umeme yangepungua kwa kiasi kikubwa kuanzia Septemba 7, mwaka huu yamekuwa kinyume chake kutokana na adha ya upatikanaji wa nishati hiyo kuongezeka.

Maeneo mengi ya Jiji la Dar es Salaam hayana umeme yapata siku tatu sasa, huku mengine yakipata nishati hiyo mara moja katika muda wa saa 36 na 48.
Ngeleja alitoa ahadi kwamba kungekuwa na nafuu ya mgawo baada ya kuwashwa kwa mitambo ya umeme ya Kampuni ya Symbion na ile ya Aggreko ambayo kwa ujumla wake, ilitarajiwa kuzalisha megawati 137.5.
Hata hivyo, hadi jana jioni mitambo hiyo haikuwa imewashwa hivyo kusababisha maeneo mengi ya Dar es Salaam kuendelea kuwa gizani.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili jana umebaini kuwa baadhi ya maeneo ya yakiwamo Ubungo, Mwenge, Kimara, Temeke, Keko na Sinza makali ya mgawo wa umeme yamezidi huku Tabata kukiwa hakuna umeme kwa siku tatu mfululizo.
Mtendaji  Mkuu wa Symbion, Stanley Munai alisema bado hawajaanza uzalishaji licha ua mafuta ya kuwashia mitambo kufika akisema kwanza wameyapeleka kuyapima ili kujua kama yanafaa ama la... “Tunasubiri majibu ili kuona kama yanafaa au hayafai.”

Alisema uamuzi wa kuyapima mafuta hayo umezingatia kwamba mtambo wao utakuwa ukiyatumia kwa mara ya kwanza, hivyo ni lazima yapimwe ili yasije kusababisha tatizo jingine.
“Ukiwasha bila kupima mafuta unaweza kuua mtambo, mafuta huwa tunachukulia katika kampuni ya kuuza mafuta ya BP,” alisema Munai.

Alipoulizwa ni lini mitambo hiyo itawashwa, Munai alisema: “ Muda wowote tu tukishapata majibu, mafuta huwa yanapimwa na kampuni ya SGS au Intertake.”

Alichoahidi Ngeleja Septemba 4
Septemba 4, mwaka huu alipotembelea mitambo hiyo iliyopo Ubungo, Ngeleja alisema makali ya umeme yangepungua kwa kiasi kikubwa akirejea ahadi aliyopewa na Symbion kwamba mitambo yao ingewashwa katika muda huo.
Ngeleja kwa kauli ya kujiamini alikwenda mbali zaidi huku akisisitiza kwamba mpaka kufikia Desemba mwaka huu, uzalishaji wa umeme utafikia megawati 572, hivyo kutamaliza kabisa mgawo wa umeme.

 “Mitambo ya Symbion ina uwezo  wa kuzalisha megawati 112 ambayo inatumia gesi na mafuta mepesi, mpaka sasa inazalisha megawati 75 tu, megawati nyingine 35.7 za mtambo huu zitaanza kuzalishwa kesho (Septemba 6) au keshokutwa (Septemba 7) baada ya kuwasili kwa mafuta mepesi” alisema Ngeleja.

Alisema kuwa mitambo ya Aggreko ambayo inazalisha megawati 100 utawashwa baada ya kukamilika kwa ufungaji wa baadhi ya vifaa zikiwemo transfoma.
Hii si mara ya kwanza kwa Ngeleja kutoa kauli kama hiyo kwani amekuwa akifanya hivyo na kutoa ahadi ambazo utekelezaji wake umekuwa mgumu.

Mapema mwaka huu, wakati akiapishwa kushika nafasi yake ya Waziri wa Nishati na Madini kwa kipindi kingine, aliutangazia umma kwamba mgawo wa umeme ungekuwa historia lakini wiki hiyo ya kwanza tangu kuapishwa kwake nchi ikatikiswa na mgawo mkubwa.

Alipotafutwa kwa ajili ya kuzungumzia ongezeko la makali ya mgawo, Meneja Uhusiano wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco), Badra Masoud hakupatikana kwani simu yake ilikuwa ikiita bila majibu ya kupokewa.

Hata hivyo, mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo ambaye hakutaka kutajwa jina lake kwa kuwa si msemaji wa alisema Badra alikuwa msibani na kwamba hayupo ofisini mpaka Jumatatu ijayo.

“Badra amefiwa hayupo kwa sasa, ila kuhusu suala la mtambo wa Symbion ungekwenda kuzungumza na haohao Symbion kwa sababu wao wanawauzia umeme Tanesco,” alisema mfanyakazi huyo.

Kuhusu mitambo ya Aggreko alisema mitambo hiyo itawashwa mwezi huu baada ya kukamilika ufundi.
“Unajua kuna upungufu wa megawati 300 katika Gridi ya Taifa kwa hiyo hata zikiwashwa hizo megawati 37.5 za Symbion na megawati 100 za Aggreko bado kutakuwa na mgawo, Waziri Ngeleja alifafanua kuwa mpaka Desemba mwaka huu ndipo mgawo utakwisha kabisa,” alisema mtumishi huyo.

Friday, September 9, 2011

TEMEKE KINONDONI NANI ZAIDI KATIKA MASUMBWI

Na Mwandishi Wetu Kambi ya Ilala

MABONDIA Mbwana Matumla wa Temeke na Francis Miyeyusho wa Kinondoni Dar es Salaam wanatarajia kupanda ulingoni katika pambano la kudhihirishiana ubabe kati ya mabondia wa Temeke na Kinondoni litakalofanyika Oktoba 30 mwaka huu.

Pambano hilo pia litafuatiwa na lingine kati ya Ramadhani Shauri wa Kinondoni dhidi ya Issa Sewe wa Temeke ambapo yote yatafanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kocha Msaidizi wa Kambi ya Kinyogoli Foundation ya Dar es Salaam, Rajabu Mhamila 'Super D' alisema mapambano hayo yameandaliwa na Promota Mohamedi Bawaziri kuhamashisha mchezo huo.

"Mabondia wote wameanza mazoezi na kwa upande wa Temeke wapo kambini chini ya Kinyogori Foundation chini ya kocha Habibu Kinyogori akishirikiana na mimi na tunawaandaa kucheza ngumi za kisasa sio kurusha ngumi bila mpangilio.," alitamba Super D

Alisema pambano kati ya Matumla na Miyeyusho litakuwa  la uzani wa Bantam Weight kilogramu 54 ambapo Shauri na Sewe watacheza kilogramu 58, uzito mwepesi (Light Weight).

Alisema licha ya kuhamasisha, kumekuwepo na tambo za mda mrefu kati ya mabondia wa Kinondoni, na wenzao wa Temeke ambapo mashabiki watajionea mapambano hayo.

Kocha huyo alisema mapambano hayo yatasindikizwa na mengine kutoka kwa mabondia wa Temeke na Kinondoni ambapo pia kutakuwepo na burudani mbalimbali zitakazotangazwa baadae.

--
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, September 7, 2011

Mchezaji Nazir Khalfan Atinga Ikulu Kumshukuru Rais Jakaya Kikwete na Kumkabidhi Jezi


 Mtanzania anaecheza Soko la Kulipwa katika timu ya White Caps ya Jijini Vancour Canada Nizar Khalfan akimkabidhi Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Jakaya Kikwete jezi ya timu anayoichezea wakati alipokwenda kumsalimu na Kumshukuru Rais Jakaya Kikwete Ikulu Jijini Dar Es Salaam.Picha na Freddy Maro-IKULU

Monday, September 5, 2011

Ikulu Yakanusha Taarifa Za WikiLeaks Kumhusu JK

By Fumbuka Ng'wanakilala


DAR ES SALAAM, Sept 5 (Reuters) - Tanzania's presidency on Monday slammed allegations in a U.S. cable that President Jakaya Kikwete accepted gifts from an investor who also donated $1 million to the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party.

A February 2006 U.S. cable published by WikiLeaks said Ali Albwardy, owner of a leading hotel chain in the east African country, flew the Tanzanian leader to London on a shopping trip and bought designer suits for the president.

"President Kikwete has accepted gifts (bribes) from the owner of the Kempinski Hotel chain's Tanzanian properties, a citizen of the United Arab Emirates," the cable reported.

"Albwardy had recently flown Kikwete to London for a subsidised shopping expedition. Among other things, on that trip Ali Albwardy bought Kikwete five Savile Row suits. He had also recently made a $1 million cash contribution to the CCM (which is a legal contribution under current Tanzanian law)."

Albwardy could not be reached for comment.

Kempinski recently ended its operations in Tanzania, with Albwardy's Kilimanjaro Hotel in the commercial capital Dar es Salaam being managed by Hyatt Hotels since August 1.

A spokesman for the president's office said Kikwete had never accepted gifts from any investor and denied that CCM was given a $1 million contribution.

"This cable is as untruthful as it is outrageous. It is full of lies and innuendoes seeking to tarnish the good image and name of the president," Salva Rweyemamu, director of presidential communications, told a news conference on Monday.

"We would like to state categorically that there has never been a time when the president received gifts from Ali Albwardy," Rweyemamu said.
"LITTLE GIFTS"

The U.S. cable comes at a sensitive time for the ruling party as it faces potential political fallout from graft allegations against some other senior members, including a former prime minister.

In May, donor countries slashed funding pledges for Tanzania's 2011/12 budget, citing concerns about corruption and the slow pace of reforms.

Some Tanzanian members of parliament recently voiced their displeasure at ongoing talks between the government and the UAE investor on handing over a building occupied by the court of appeal to the Kilimanjaro hotel for an expansion project.

Albwardy owns three hotels in Tanzania -- the Kilimanjaro Hotel, a beach hotel in Zanzibar and a lodge in the Serengeti national park -- through the company Albwardy Investment.

The Kilimanjaro Hotel was the country's flagship state-owned hotel until it was sold to Albwardy in 2002, under the previous CCM administration. Kikwete came to power in 2005.

The leaked files show the former U.S. ambassador to Tanzania, Michael Retzer, was given the allegation about the presidential gifts by a former director of the Kilimanjaro Hotel.

"Kikwete probably believes there is no harm in taking these 'little gifts' to do what he would have been inclined to do anyway. That said, they are what they are: bribes," the U.S. cable stated.

Rweyemamu said the former director quoted in the U.S. embassy cable as the source of the information had sent an email to the Tanzanian government dismissing the report as "absolutely not true and a complete load of rubbish".

Rweyemamu also said the Tanzanian president blocked plans by the UAE investor to build another hotel at the Ngorongoro crater due to environmental concerns.

"If the president indeed received such generous gifts from Albwardy, how could he have rejected the Ngorongoro project?" He said.

KAMATI TEULE YA BUNGE KUMCHUNGUZA JAIRO YAANZA KAZI LEO





Wajumbe wa Kamati Teule iliyoundwa na Bunge kuchunguza sakata la aliyekuwa
katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Ndg. David Jairo kuchangisha pesa kwa
ajili ya kupitisha Bajeti ya Wizara pamoja na hatua ya katibu Mkuu kiongozi
kuitolea taarifa ya uchunguzi mbele ya waandishi wa Habari kabla ya kuwasilishwa
Bungeni imeanza kukutana leo katika Ofisi ndogo ya Bunge chini ya uenyekiti wa
Mhe. Injinia Ramo Makani (CCM), mbunge wa Tunduru Kaskazini,
.
kamati hiyo inayoundwa na mhe. Goesbert Blandes (CCM), Mbunge wa Karagwe, mhe.
Mchungaji Israel Natse (Karatu-Chadema), mhe. Khalifa Suleiman Khalifa
(Gando-CUF) na mhe. Martha Jachi Umbulla (CCM). Mbunge wa Viti Maalum, inafanya
kazi kwa kuongozwa na hadidu tano za rejea ambazo ni:

kuchunguza utaratibu uliobainika wa kukusanya fedha kwa ajili ya kukamilishwa
kwa uwasilishaji wa Hotuba za bajeti za wizara bungeni na kwamba, hadidu hiyo ya
kwanza itakuwa na vipengele vitatu. Vipengele hivyo ni pamoja na: kuchunguza uhalali wa utaratibu huo kisheria na kwa mujibu wa kanuni, iwapo
fedha hizo huwa zinakasimiwa katika bajeti husika pamoja na matumizi halisi ya
fedha zilizokusanywa.

Hadidu rejea ya pili ni kupitia taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali kuhusu uchunguzi alioufanya kuhusiana na agizo la Katibu Mkuu wa Wizara
ya Nishati na Madini kuchangisha fedha taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kwa
ajili ya kufanikisha uwasilishaji wa Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni,

Hadidu rejea ya tatu ni kuchunguza mfumo wa Serikali kujibu hoja zinazotolewa
bungeni na taratibu za kuarifu Bunge matokeo ya utekelezaji wa hoja hizo".

Hadidu rejea hiyo ya nne ina vipengele viwili ambavyo ni kuchunguzwa kwa usahihi
wa utaratibu uliotumiwa na Katibu Mkuu Kiongozi kwa suala la Jairo na kubaini
iwapo utaratibu huo umeathiri dhana ya haki na madaraka ya Bunge.

Hadidu ya rejea ya tano ni kuangalia nafasi ya Mamlaka ya Uteuzi kwa ngazi za
Makatibu Wakuu katika kushughulikia masuala ya nidhamu ya anaowateua na ya
mwisho inawaelekeza wajumbe wa Kamati hiyo kuangalia mambo mengine yoyote yenye
uhusiano na uchunguzi huo.

Picha na Habari: Owen Mwandumbya wa Bunge

Saturday, September 3, 2011

CCM Yapeta Katika 'Uchaguzi Mwenyekiti Wa Halmashauri Ya Rungwe



CHAMA cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Rungwe mkoa wa Mbeya kimeshinda kwa kishindo nafasi ya mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Rungwe kwa kuwabwaga  wapinzani katika uchaguzi huo mdogo.Uchaguzi huo ulifanyika ili kuziba pengo liloachwa wazi na aliyekuwa mwenyekiti wa halmashauri hiyo aliyeuwawa mwanzoni mwa mwaka huu kwa kupigwa risasi.
Habari kutoka Rungwe zinaripoti kuwa katika uchaguzi huo wajumbe wamemchagua kwa kura 40 aliyekuwa makamu mwenyekitiwa halmashauri hiyo, Meckson Mwakipunga (pichani) huku mgombea wa NCCR Mageuzi,Anyimike Mwakasikilali akiambulia kura 3 tu. (francisgodwinblog)

Wednesday, August 31, 2011

Rais wa Zanzibar Dk.Ali Shein Ahudhuria Swala ya Idd el Fitri Bwawani Hotel Zanzibar


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk Ali Mohamed Shein,akiwahutubia wananchi na waislamu katika baraza la Iddi el Fitri lililofanyika huko ukumbi wa Salama hall Bwawani Hotel mjini Zanzibar.
Makamo wa kwanza wa Rais Seif Sharif Hamadi akisalimiana na Waziri wa katiba na Sheria wa Zanzibar Abubakari Khamis Bakari baada ya kuingia katika kiwanja cha maisara mjini zanzibar kwa ajili ya kuswali swala ya Idi Elfitri.
Rais wa Zanzibar Alhaji Dr,Ali Mohd Shein pamoja na viongozi mbalimbali wa vyama na serikali na wananchi,wakiwa katika swala ya iddi ambayo imeswaliwa kitaifa katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar.
Baadhi ya kinamama waliohudhuria katika swala ya Idi Elfitri huko katika kiwanja cha Maisara mjini Zanzibar
 Wananchi mbalimbali wa Zanzibar wakisikiliza hotuba ya Idi Elfitri baada ya kumaliza kuswali swala ya Idi huko katika kiwanja cha maisara zanzibar.Picha na Ramadhan Othman wa Ikulu -Zanzibar

Monday, August 29, 2011

Mbunge Wa Mvomero Aingilia Kati Mgogoro Wa Ardhi Kipera

|
Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makala akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero, Morogoro mwishoni mwa wiki katika harakati za kutatua mgogoro wa ardhi uliopo kijijini hapo , kufuatia mwekezaji Raia wa kigeni kuuziwa eneo kubwa la ardhi na kumega sehemu ya mashamba yao, kufunga barabara, shule na kubomoa baadhi ya vyoo vya wakazi wa kijiji hicho. MBUNGE wa jimbo la Mvomero, mkoani Morogoro, Amos Makala ameingilia kati mgogoro wa ardhi uliopo katika Kitongoji cha Kinyenze , Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali , Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro baina ya wananchi na mwekezaji wa Kigeni aliyeuziwa shamba kijijini hapo.

Akizungumza mwishoni mwa wiki Kijijini hapo Makala aliyeambatana na Ofisa Ardhi wa Wilaya hiyo, Majaliwa Jaffari amewataka idara ya ardhi kuchukua hatua za haraka na dharula kutatua mgogoro huo kabla ya kuibuka kwa machafuko ya uvunjifu wa amani.

“Nimejionea mwenyewe baada ya kusikia kiliochenu juu ya mwekezaji huyu, watu wa ardhi tafadhalini sana lishughulikieni suala hili haraka sana na mkae pamoja mgogoro huu umalizike upesi iwezekanavyo, ndani ya wiki moja tatizo hili liwe limemalizika”, alisema Makala.

Aidha Makala amesema tatizo hilo likiendelea ataungana na wananchi wake kufungua kesi Mahakamani ya kumpinga mwelezaji huyo na amemwomba Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero kutumia mamlaka waliyonayo kufika kijijini hapo wafungue uzio huo uliowekwa na mweklezaji huyo haraka ili kuwawezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za uzalishaji mali, watoto kwenda shule na watu kuvuna mazao yao yanayoibiwa na walinzi wa kampuni ya Tanbreed Poultry Limited ambayo imemega mashamba yao.

“Katika hili ninaungana nanyi na Viongozi wa Mkoa na Wilaya wafike hapa wakiwa na dola na kukata uzio huu, ili wananchi muendelee na shughuli zenu za kijamii, si haki kufunga barabara mnayoitumia kwenda katika makazi yenu na mashambani, hili lisipofanyika tutatafuta mwanansheria na kufungua kesi ya Mahakamani ya kumpinga mwekezaji huyu”,alisema Mbunge Makala.

Makala pia aliwapongeza wakazi wa kijiji hicho kwa kuwa watulivu pasipo kufanya vurugu katika kipindi kirefu tangu kuibuka kwa mgogoro huo bila kupatiwa ufumbuzi kutoka kwa viongozi wa ngazi za juu licha ya kuandikiwa barua tangu mwezi Aprili mwaka huu mgogoro huo ulipoanza kushika kasi.

“Wananchi mmefanya jambo jema sana la kuheshimu mamlaka za kisheria kwa kuwa watulivu kipindi chote lakini vinginevyo hapa machafuko yangetokea maana wananchi mpo wengi kuliko hao askari wao wanaolinda hilo shamba”, alisema Makala.

Pia alisema kwa maelezo aliyoyasikia kutoka kwa baadhi ya wazee wa kijiji hicho Ally Kidunda na Said Ahmad na viongozi wa Kijiji yaliyotolewa kwaa nyakati tofauti Mwekezaji huyo ndiye mvamizi wa eneo lao na si wananchi maana hata kijiji hakimtambui kwa maana hajawahi kufika kwao.

Nae Ofisa Ardhi wa Wilaya ya Mvomero, Majaliwa Jaffari alisema watalishughulikia suala hilo haraka na hasa baada ya kufika eneo la tukio na kukiri kuna mapungufu katika ramani waliyonayo.

Agosti 23, mwaka huu wananchi hao waliitaka serikali kuingilia kati mgogoro huo haraka kabla ya machafuko kutokea wakati wakiwa katika mkutano wa hadhara uliokuwa uhudhuriwe na Mkurugenzi wa Wilaya na Maofisa wa Ardhi. Habari na Picha:Mroki Mroki

Monday, August 15, 2011

SOBER HOUSE YATEMBELEWA NA MAAFISA WA MADAWA YA KULEVYA



Mmoja katika vijana waliopo Sober akielezea uamuzi wake wa kujiunga na Sober House kuachana na madawa na jinsi anavyoendelea kupata ushauri nasaha, dawa pamoja na maelezo
Viongozi waadamizi wa kitengo cha Madawa ya kulevya wakisikiliza kwa utulivu maelezo yaliyotolewa na waratibu pamoja na waathirika wa madawa ya kulevya katika ziara yao kujifunza jinsi ya kupunguza matumizi ya madawa Zanzibar
Vijana wa Sober house tawi la Tomondo wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa waandamizi wa madawa ya kulevya.
Mimi pia nikuwepo wakati wa picha ya pamoja pamoja na kamkoba changu kwani nilipomaliza tu nilikimbilia kwenda kutafuta futari.Picha Zote na Mdau Othman Mapara

Friday, August 12, 2011

Adha Ya Mgomo Wa Wauza Mafuta

Treni yasitisha safari kwenda bara
*Nauli, vyakula mikoani bei zapanda
*Wachumi watabiri hali mbaya zaidi
UPUNGUFU wa mafuta katika maeneo mbalimbali nchi umezidi kukolea na kusababisha athari mbalimbali za kiuchumi, ikiwamo kusitishwa kwa safari za treni ya kati, kupanda kwa nauli na bei za vyakula, huku wachumi wakitabiri hali mbaya zaidi.
Safari za treni kusitishwa
Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) imesitisha safari za treni ya abiria kutoka Dar es Salaam kwenda bara kutokana na kukosa mafuta.
Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo, Bw. Midladjy Maez alisemsa jana kuwa kutokana na hatua hiyo, treni iliyokuwa imepangwa leo saa 10:00 jioni kwenda bara na iliyopangwa kuondoka Tabora kwenda Mpanda kesho hazitakuwapo.


"Kampuni imeamua kusitisha safari za treni za abiria kwenda bara kutokana na maghala yetu kukosa mafuta ya kutosha, hivyo safari zitarejea endapo zitapata mgawo wa kutosha wa nishati hiyo," alisema Bw. Maez.
Aliwataka watu wote waliokata tiketi za kuondoka kwenda maeneo hayo kuonana na wakuu wa vituo ili kurejeshewa nauli zao, huku akiomba wawe wavumilivu katika kipindi hiki kutokana na usumbufu wanaoupata.
Mbeya nauli juu
Tatizo hilo la mafuta nchini limechukua sura mpya baada ya wamiliki wa daladala mkoani Mbeya kupandisha nauli kutoka sh. 350 mpaka 500 kutokana na nishati hiyo kupandishwa hadi sh. 3,000 kwa lita moja.
Wakizungumza na gazeti hili jana kwa nyakati tofauti, wakazi wa eneo la Uyole jijini Mbeya walisema kuwa kiwango hicho cha nauli kimepanda bila kuzingatia utaratibu huku magari mengine yakishindwa kufanya kazi.
Mkazi wa Uyole, Bw. Ablahamu Kazubele alisema kuwa nauli ya awali kutoka Uyole kwenda mjini ilikuwa sh. 350 na sasa imekuwa sh. 500 ambayo si ya kawaida.
Dereva wa daladala inayofanya kazi zake kati ya Uyole na Igawilo maarufu kwa jina la Mwagito alisema kuwa wao wamelazimika kupandisha nauli kutokana na mafuta kupanda bei hadi sh. 3,000 kwa wachuuzi mitaani.
Vyakula vyapanda bei Songea
Mkoani Ruvuma, mgomo huo umesababisha kupanda bei kwa kilo ya unga kutoka sh. 600 hadi 1,500 na mchele kutoka sh. 1,000 hadi sh. 1,500 katika manispaa ya Songea.
Bw. Rashidi Hussein mkazi wa eneo la Mpambalioto mjini hapa alisema kuwa tatizo la kutokuwepo kwa dizeli na petroli limeleta athari kubwa, hasa kwa waumini wa dini ya kiislamu ambao kwa sasa wako katika mfungo wa Ramadhani.
Naye Bw. Didas Lyakulwa maarufu kwa jina moja la Mabrandi, alisema:
“Ndugu waandishi leo nimenunua mafuta ya petroli lita mojash. 5,000 badala ya sh. 2,135 kwa lita, kwa ajili ya kuweka kwenye jenereta ninalotumia kwenye biashara yangu ya baa na hoteli, hivyo kupata hasara kubwa,” alisema Bw. Lyakulwa.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dkt. Christine Ishengoma alisema tayari ameshawaagiza wamiliki wa vituo vyote vya mafuta mkoani humo wahakikishe kuwa mafuta yanapofika wayauze kwa bei halali, vinginevyo watachukuliwa hatua.

Wachumi watabiri mabaya
Wakati huo huo, wachambuzi wa masuala ya uchumi na siasa wametahadharisha kuwa kama tatizo hilo na mgawo wa umeme havitatatuliwa kwa njia sahihi, uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja utaendelea kuporomoka.
Wachumi hao wamesema kuwa wananchi wajiandae kwa hali ngumu ya maisha, ikiambatana na ukosefu wa ajira kuliko ilivyo sasa.Profesa Samuel Wangwe alisema kuwa ni wakati mwafaka sasa serikali ijue kwa undani namna biashara ya mafuta inavyoendeshwa, ili siku nyingine isikurupushwe kama inavyoonekana kutokea hivi sasa.
"Kama hali hii itaendelea, kwa kweli kutakuwa na tatizo kubwa, vitu kutofika, gharama za kusafirisha, kupanda kwa bei za vitu...hili la ulanguzi linaloonekana sasa ni matokeo tu ya upungufu huu wa mafuta.
"Lakini ni vyema serikali ikaijua vyema biashara hii, si kama sasa hivi ambapo inaonekana imekuwa taken by surprise. Waelewe biashara hii inakwendaje, imekaaje, wajue serikali inapaswa ku-play role gani hasa katika biashara ya mafuta, wadhibiti wakiwa na taarifa kamili ya nini kinafanyika. Wajifunze katika hali kama hii, nchi zingine kama Ujerumani, Sweden, Marekani au Uingereza zinafanyaje katika kuhakikisha inafanya kazi kwa ufanisi.
Kwa upande wake Profesa Ibrahim Lipumba alisisitiza kauli yake amabyo amekuwa akiitoa mara kwa mara juu ya ombwe la uongozi, ambalo alisema limekuwa likionekana katika serikali iliyoko madarakani, akiongeza kuwa kama ufumbuzi sahihi hautapatikana kwa wakati mwafaka taifa na wananchi kwa ujumla watakuwa katika matatizo makubwa kuliko ilivyo sasa.
Prof. Lipumba ambaye yuko katika mapumziko ya kujenga afya yake baada ya kufanyiwa operesheni nchini India hivi karibuni, aliungana na Prof. Wangwe, akisema kuwa kama hakutakuwa na suluhisho la haraka, kutakuwa na mfumuko mkubwa bei kuliko ilivyo sasa, hivyo kusababisha hali ya maisha kuzidi kuwa ngumu.
"Tatizo ni hilo hilo ambalo mara kwa mara tumelisema, bahati mbaya na ninyi ujumbe mmekuwa hamuufikishi sawa sawa kama inavyotakiwa. Suala la mafuta limedhihirisha ombwe la uongozi ambalo nimekuwa nikisema. Suala la kupunguza bei lilifanywa kisiasa zaidi kwa ajili ya kujipatia umaarufu. Inavyoonekana serikali haikufanya utafiti kabla, kuwasiliana na wauzaji kabla ya bajeti.
"Serikali ilipaswa kujua mapema kuwa utaratibu mpya hautakuwa na athari yoyote...leo kuna mtu kaniambia bei za bajaj zimepanda, sasa mafuta yanaanza kuuzwa kwa bei ya magendo kwa bei ya kuruka...matatizo yatakuwa makubwa zaidi kuliko ilivyo sasa. Hakuna sheria inayowapatia EWURA mamlaka ya kupanga bei, wanaweza kutoa bei elekezi tu, ingawa pia wauzaji hawaruhusiwi kupanga njama za kuuza bei kubwa maana hiyo ni jinai.
"Kwa sababu hakuna price control huwezi kuwashtaki, bali unaweza kuwanyang'anya leseni wasiuze mafuta tena. Lakini serikali ilipaswa kulifanyia suala hili utafiti kabla hata ya bajeti, kujua kama uamuzi huo ungeweza kuongeza matatizo zaidi. Serikali lazima ifanye mambo kwa uhakika. Na katika hali ya sasa ujue hata meli zinaweza kuelekezwa kupeleka mafuta sehemu nyingine badala ya kuleta Tanzania, hivyo tukaendelea kuwa katika matatizo makubwa."
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. John Heche alidai kuwa anazo nyaraka zinazoonesha kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kina mikataba ya kibiashara na baadhi ya makampuni ya mafuta, ndiyo maana hakiwezi kukemea hali inayoendelea nchini, huku pia akisema kuwa baadhi ya wabunge na mawaziri wana mgongano wa maslahi katika tatizo hilo.
"Ninazo nyaraka, nitazitoa wakati mwafaka, CCM wana mikataba ya kibiashara na baadhi ya makampuni ya mafuta, mmoja una kiasia cha sh. bilioni 3. Hiyo ni mbali na kuwa uongozi wa sasa wa serikali ya CCM uliingia kwa ufadhili wa fedha za makampuni hayo, ndiyo maana mpaka sasa hatujasikia kauli 'serious' juu ya suala hili.
Akizungumzia shutuma hizo, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Bw. Nape Nnauye alisema "mwambieni Heche azitoe hizo nyaraka, maana sasa hivi ndiyo wakati mwafaka, suala la mafuta linazungumzwa sana, atoe tu. Sisi tunaweza kutoa mikataba yote, ingawa unaweza kumtafuta Mwigulu Nchemba, maana yeye ndiyo hasa anahusika na Idara ya Fedha na Uchumi, anaweza kukwambia mengi.
"Lakini hayo ni maneno ya kihuni, yamekuwa yakitolewa na watu mbalimbali, nimeyaona hata mtandaoni...lakini hata maneno kuwa hatujachukua hatua...ukiuliza sisi ndiyo tulikuwa tunahangaika kuhakikisha mambo yaende. Mpigie Mwichemba atazungumza zaidi."
Majira lilimtafuta Bw. Nchemba kwa simu yake ya mkononi lakini ilikuwa ikiita bila kupokewa, hivyo ikalazimu kumtumia ujumbe mfupi, kumwomba azungumzie shutuma hizo, lakini hatukupata majibu hadi tunakwenda mitamboni.
Imeandikwa na Esther Macha, Mbeya; Cresensia Kapinga, Songea; Tumaini Makene na Grace Ndossa.

Thursday, August 11, 2011

Matukio Bungeni ...


Zainab Kawawa (shoto) vitimaalum (kulia) Angelah Kairuki (CCM) vitimaalum wakiteta...

Waziri Mkuu (mwenyetai ya zambarao) akiongea na wasanii Bungeni ...

Mdau wa Habari Neville Meena (kulia) akimpongeza waziri nchmbi katika viwanja vya bunge. Picha zote; Mwanakombo Jumaa, HABARI MAELEZO

Tuesday, August 9, 2011

Rais Wa Somalia Atua Tena Tanzania

Rais Jakaya Kikwete (kulia) akikumbatiana na mgeni wake Rais Sheikh Sharif Ahmed wa Jamhuri ya Somalia alipowasili jana mchana kwa ziara ya kikazi ya siku mbili nchini.
Rais Jakaya Kikwete na mgeni wake Rais Sheikh Sharif Ahmed wa Jamhuri ya Somalia wakipita katikati ya gwaride la mapokezi ya mgeni huyo mara baada ya kuwasiri kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.

Dr Shein Azindua Uchumaji Wa Karafuu ...

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohammed Shein akipima karafuu katika uzinduzi wa Uchumaji wa zao hilo huko Mkanyageni Pemba...


Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein akianika Karafuu pamoja na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Nassor Ahmed Mazrui katika siku ya uzinduzi wa Uchumaji wa zao hilo Msimu huu huko Pemba.

Saturday, August 6, 2011

CCM Itarejesha Imani Ya Vijana, Na Kuwaeleza Ukweli Ulivyo-Nape


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kitahakikisha katika mabadiliko yake ya sasa kinawarejesha katika kuujua ukweli vijana waliopotoshwa na wapinzani hadi kufikia hatua ya kudhani hakuna mazuri yaliyofanywa tangu uhuru.


Mikakati hiyo ilisemwa jleo na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye wakati akizungumza na baadhi ya viongozi na watangazaji wa Clouds Media Group, Mikocheni Dar es Salaam, alipofanya ziara ya kujitambulisha katika wadhifa wake huo na kueleza mabadiliko yaliyofanywa na Chama, mapema Aprili mwaka huu.


Alisema, wakati wapo vijana ambao hawakuipigia kura CCM katika uchaguzi mkuu uliopita kwa sababu zinazoonekana kuwa za msingi, lakini ipo idadi kubwa ya vijana ambao walifanya hivyo kutokana na chuki tu kutokana na kushibishwa na uongo na baadhi ya vyama vya upinzani.


Nape alisema katika miaka ya karibuni hasa baada ya kupevuka kwa kiwango kikubwa mawasiliano kwa njia ya mitandao kwenye kompyuta, baadhi ya vyama hivyo vimetumia na vinaendelea kutumia mawasiliano hayo kueneza uongo kwa njia hiyo na kufanikiwa kuwanasa vijana wengi kwa kuwa ndio wanaopendelea zaidi kutumia mawasiliano hayo ya mtandao.


"Baada ya vyama vya upinzani kujua kwamba vijana wengi wanapenda zaidi upashanaji habari kwa njia ya mitandao kwenye kompyuta, kuliko mikutano ya hadhara na njia nyingine za kawaida,


baadhi ya vyama hivi vimetumia sana njia hii kuwajaza uongo vijana", alisema Nape.


"Na kwa sababu uongo ukizidi kuenezwa bila kupingwa huweza kuonekana ndiyo ukweli, baadhi ya vijana wameamini uongo huo, na matokeo yake wamejenga chuki kiasi cha kutoyaamini hata mambo ya maana na ya msingi wanayoambiwa na CCM na serikali yake jambo ambalo ni hatari kwa hatma ya taifa", alisema Nape.


Alisema katika mikakati yake ya sasa CCM itahakikisha inawapa ukweli kupitia njia hiyo ya mawasiliano ya mitandao ya kwenye kompyuta kama 'face book' na kueleza matumaini yake kwamba hatua hiyo itazaa mafanikio kwa kuwa yameanza kuonekana katika hatua za awali ambazo CCM imeanza kufanya.


Nape alisema, CCM inafanya hivyo kwa kuwa bado kina uwezo wa kuongoza huku kukiwa hakuna chama cha upinzani ambacho kinaweza kujitapa kuwa kinaweza kuongoza nchi kwa uhakika ikilinganishwa na hali inayojionyesha katika vyama hivyo hadi sasa.


Alisema, mbali ya kuyaendea makundi ya vijana, CCM pia imejipanga kuyafikia kwa ufanisi zaidi makundi yote, kwa kutumia njia mbadala, ikiwemo kufuatilia kwa karibu maoni ya vyombo vya


habari hasa vile vinavyoonekana kuwa makini zaidi katika kutoa habari zake.


Nape aliahidi CCM kutoa ushirikiano mkubwa kwa vyombo vya habari katika kuhakikisha vinapata habari za ukweli, sahihi na kwa wakati kuhusu chama na hata za ndani ya serikali.


"Tunaamini sisi CCM tukifungua masikio yetu vilivyo kwa vyombo vya habari tuyaweza kuongoza nchi kwa usahihi zaidi, kwa sababu ninyi vyombo vya habari ndiyo mliopo mitaani wakati mwingi, hivyo mnaweza kuwa mnayajua mengi kuliko sisi, ni vizuri tukawa tunawasikiliza na kufanyia kazi mnayosema", alisema Nape.


Katika ziara hiyo, Nape alizungumzia kwa kina dhana ya mabadiliko ndani ya Chama na utekelezwaji wake unavyoendelea na baadaye waandishi wa Clouds Media Group walipata fursa ya


kuzungumza na kumuuliza maswali yaliyoona yanafaa.


Baadaye Nape akiongozwa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa kampuni hiyo ambayo ni walimiki wa vituo vya Clouds FM, Choice FM na Clouds TV, Ruge Mutahaba alipata fursa ya kutembelea baadhi ya vituo hivyo kuona kazi zinavyofanyika.

Balozi Wa Zambia Nchini Amtembelea Rais Wa Zanzibar Dk Ali Shein

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akifuatana na mgeni wake Balozi wa Zambia nchini Tanzania Mama Mavis Lengalenga Muyunda, aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar Leo kuzungumza na Rais
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi wa Zambia nchini Tanzania Mama Mavis Lengalenga Muyunda aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar Leo.Picha na Ramadhani Othman,Ikulu-Zanzibar

Thursday, August 4, 2011

Mhe.Lowasa Ziarani India



Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Edward Lowassa


MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Edward Lowassa (katikati kulia) akiwa katika kikao cha pamoja na Wabunge wa Bunge la India wanaoongozwa na Spika wa Bunge lao, Lok Sabha . Kikao hicho kilifanyika New Delhi India ambako kamati hiyo iko katika ziara ya kikazi.

Tuesday, August 2, 2011

Bada Ya Kamati Kuu Ya CCM Kulalamikia Bei Ya Mafuta, Bei Za Mafuta Zapungua

Serikali imepuguza bei ya mafuta ili kuwapunguzia makali watumiji wa badhaa hiyo nchini.


Akizungumza na wanahabari Mkurugenzi wa EWURA Haruna Masebu amesema mafuta ya petrol yamepungua kwa sh 202.37 sawa na asilimia 9.17 ambapo mafuta ya dizeli yatakuwa yamepugua kwa shilingi 173 ambay ni sawa na asilimia 8.32.


Bwana Masebu alisema alisema bei ya mafuta ya taa imeshuka kwa shilingi 181.37 sawa na asilimia 8.70 na mabadiliko hayo yametokana na marekebisho ya yaliyofanywa na kanuni kukokotolea bei za mafuta.


Alisema bei zingeshuka kwa sababu ya kupanda kwa bei katika soko la dunia na kuendelea kushuka kwa tahamani ya shilingi ya Tanzania ikilinganishwa na dola ya Marekani.


Aidha Masebu alisema, kwa mujibu wa Sheria ya mafuta ya mwaka 2008 bei za mafuta ya petrol I zitaendelea kupangwa na soko na EWURA itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo ya bidhaa za mafuta.


Alisema kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa za mafuta ya petrol kwa bei ya ushindani pasipo kuongeza bei iliyopangwa na taasisi ya EWURA.


Pia vituo vya mafuta vimetakiwa kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana ili kuonyesha bei ya mafuta.


Kwa mujibu wa Bwana Masebu bei hiyo ya mafuta imeanza kutumika rasmi leo.

Ndugai Atetea Mikopo Ya Mashangingi


Amesema badala yake wakae pamoja na kupendekeza njia ambazo zinaweza kutumika serikalini ili ununuzi wa mgari katika idara na taasisi zake mbalimbali upungue kwa lengo la kupunguza gharama za uendeshaji na matumizi makubwa ya fedha za umma. Bw. Ndugai ambaye pia ni Mbunge wa Kongwa (CCM), alitoa wito huo juzi katika mahojiano na gazeti hili Mjini Dodoma juu ya mashangini hayo ambayo yamekuwa yakilalamikiwa na wananchi. “Hamna mbunge hata mmoja ambaye anatumia fedha za umma kununulia gari la kufanyia kazi, iwe ni kutoka upinzani au chama tawala, kinachofanyika wabunge wote wanapewa mikopo ambayo inasimamiwa na Ofisi za Bunge kwa kuwapa dhamana wakati wa kwenda kukopa fedha hizo ili waweze kununua magari ya kufanyia kazi,” alisema na kuongeza: “Ofisi ya Bunge inahusika na dhamana tu, kinachofuatia ni mbunge kujaza fomu husika na kufuata taratibu zote za kukopa fedha za gari. Kwa safari hii zinatakiwa zisizidi sh. milioni 60, kati yake sh. milioni 45 ndizo wanakopeshwa na kupitia mishahara yake na posho zitakuwa zinakatwa kidogo kidogo hadi miaka mitatu awe amemaliza kurejesha,” alifafanua Bw. Ndugai. Alisema utaratibu unaotumika hapa nchini kwa kuwakopesha wabunge fedha za kununulia magari ya kufanyia kazi ni mzuri tofauti na nchi jirani kama Kenya na Uganda ambazo zinawapa bure wabunge wote kila mmoja gari lenye thamani ya sh. milioni 200. “Tumekuwa tukiwabebesha wabunge mizigo mizito mara kwa mara likiibuka suala la posho, magari, mishahara wao tu ndiyo wanaonekana wanapendelewa, lakini siyo kweli ndiyo maana serikali kwa kutambua nafasi yao katika kulitetea taifa inawajengea uwezo wa kujitegemea katika magari, kwa kuwa utaratibu wa kumkopesha mbunge gari inaipunguzia serikali gharama ya kununua magari mengi, gharama za matengenezo, mafuta na dereva wa kuwaendesha kwenda katika shughuli zao,” alisema Bw. Ndugai. Kuhusu magari ya serikali Alisema kama serikali itaanzisha utaratibu wa kuwakopesha watendaji wake fedha za kununulia magari yao binafsi ili ipunguze gharama, ikiwa ni pamoja na Wakuu wa Wilaya na Mikoa, hatua hiyo itaokoa fedha nyingi za umma. “Nimewahi kutembelea katika Wizara moja ya Mazingira nchini Afrika ya Kusini nikakuta ina magari mawili tu kwa ajili ya dharura, lakini hapa nyumbani suala hilo halipo, hivyo ninaona kama tunaweza kuiga wenzetu kwa kuwakopesha fedha ambazo zitakuwa zinarejeshwa kwa awamu na hivyo kupunguza gharama serikalini kama Rwanda ilivyowahi kufanya kwa kuuza asilimia kubwa ya magari ya serikali,” alifafanua Bw. Ndugai. Bw. Ndugai aliongeza kuwa umefika wakati kwa kila mwananchi kuliamini bunge lao kwa kuepuka maneno ya upotoshaji ambayo wakati mwingine yanaweza kuwafanya kugawanyika katika makundi mbalimbali, bali washirikiane na wabunge wao katika kuwawasilishia kero zao ili zipatiwe ufumbuzi bila kujali itikadi zao za chama.Chanzo Gazeti Majira
NAIBU Spika, Bw. Job Ndugai amewataka wananchi kuacha kuwashambulia wabunge juu ya magari wanayonunua kwa mikopo kwa kuwa kufanya hivyo wanakuwa hawawatendei haki.